DEAL PLUS

Karibu DEALPLUS BLOG uweze kupata habari za Michezo, Siasa, Afya na Burudani kutoka ndani na nje ya nchi.

Breaking


Saturday 22 July 2017

TATIZO LA KUTOPATA/KUKOSA CHOO

Hili ni mojawapo ya tatizo ambalo wengi hupenda kuliongelea na mara nyingi kwa wale ambao wameshakutwa na tatizo hili wanajua ni jinsi gani unaumia unapopata choo na ni jinsi gani unakua hupendi kuona unabanwa na haja.

Mwanadamu anatakiwa kupata choo angalau mara 1 kwa siku lakinni ratiba ya kupata choo kwa mwanadamu hutofautiana kulingana na mtu. Na hili linakua ni tatizo kwa upande mkubwa sana pale mahudhulio ya chooni kwa mwanadamu kuwa ni ya kulegalega na yasiyokua na mpangilio maalumu kwani ni wataalamu wanasema mwanadamu anatakuiwa kwenda haja kila baada ya chakula kuingia mwilini, kwa maana kwamba kama unamilo 3 basi unatakiwa uende chooni mara 3, na kama hali hiyo haitokei basi angalau kila baada ya masaa 18 adi 24, na zaidi ya hapo ilo linakua ni tatizo.

VISABABISHI NI VIPI?
Constipation hili ni neno la kilatini lenye maana ya KUSANYIKA PAMOJA.
Tatizo hili husababishwa na kutokueleweka kwa ratiba ya kwenda haja (kubwa), na mfululizo wa kutokwenda haja basi husababisha mrundikano mkubwa wa chakula baki kwenye utumbo mpana na kinachosafiri taratibu sana hivyo kusababisha mrundikano mkubwa wa chakula baki na kusababiisha ugumu sana wakati wa kutoka.

Pia vitu vingine vinavyosababisaha ni pamoja na;
Kuto kunywa maji mengi
Kutokula vyakula vinavyosaidia mfumo wa chakula mfano matunda kwa wingi na mboga za majani.
Kuvurugika kwa ratiba nzuri ya chakula hasa kwa wale wasafiri wa mara kwa mara.

Kutokufanya mazoezi nako kunachangia sana.
Msongo mkubwa wa mawazo (Stress)
Kujirazimisha kutokupata choo
Unywaji wa dawa hovyo pasipo kufata ushauri kutoka kwa wataalamu.

Kula chakula bila kufuata utaratibu wa rishe bora.
Madonda ya tumbo,
Pia kwa wanawake wajawazito hii hali huweza kutokea.

DALILI ZAKE NI ZIPI?
Na dalili za ugonywa huu ( Constipation ) ni pamoja na;
-Kutokupata haja kwa wakati.
-Kupata haja iliyo ngumu sana tofauti na kawaida.
-Tumbo kuunguruma sana.
-Na wanaume wengi wanaokua na tatizo hili la tumbo kuunguruma sana basi ujue kwamba chakula kilichopo tumboni huwa hakimen’genywi vizuri na kama chakula hakimeng’enywi vizuri basi wanaume hao huandamwa sana na tatizo la nguvu za kiume na kutoshiriki vizuri tendo la ndoa, kwani wataandamwa sana na mambo yafuatayo;

1. Kuwahi kufika kileleni.
2. Kushindwa kurudia tendo pale wanapomaliza tu mara ya kwanza,
3. Kuandamwa na uchovu mkubwa sana baada tu ya kumaliza tendo.
4. Kushindwa kusimama vizuri wakati wa tendo.
5. Kulegea wakati wakiendelea na tendo.

MADHARA YAKE NI YAPI?
Madhara ya ugonjwa huu ( constipation ) ni pamoja na;
1. Wanaume kushindwa kushiriki vizuri tendo la ndoa.
2. Kuandamwa na maumivu makali sana wakati wa kupata choo.
3. Kupata magonjwa mbalimbali ya bacteria kwa sababu ya mrundikano mkubwa wa chakula taka ndani ya utumbo mpana.
4. Kuchanika kwa kuta za puru ( Anal), kwani kunakua na mrundikano wa chakula taka ndani ya utumbo mpana na kutoka kwake husababisha kuchanika kwa kuta hizo

No comments: