DEAL PLUS

Karibu DEALPLUS BLOG uweze kupata habari za Michezo, Siasa, Afya na Burudani kutoka ndani na nje ya nchi.

Breaking


Saturday 23 September 2023

September 23, 2023

AJALI YA ROLI YAUA WATU 9

 


 

WATU tisa wamefariki dunia mkoani Mbeya baada ya  dereva wa lori lenye namba za usajili BCE 9384/ABX8675 kushindwa kulimudu gari lake kwenye mtelemko mkali  wa Mbalizi na kwenda kuigonga gari ya abiria na yenye namba za usajili T.636 DQY aina ya Mitsubishi Rosa .

 Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Mbeya,Benjamin Kuzaga amesema kuwa tukio hilo limetokea Septemba 22 mwaka huu majira ya saa 11.40 jioni  katika eneo la mteremko wa Iwambi wilaya ya Mbeya Vijijini  mkoa wa Mbeya .

Kamanda Kuzaga amesema kuwa gari  yenye namba za usajili BCE 9384/ABX 8675 aina ya Howo mali ya kampuni ya Horn Afric Motors ltd ya nchini Zambia ikitokea Mbeya kuelekea Tunduma likiendeshwa na dereva Mohamed Abilah (47) Mkazi wa Zambia .

Aidha Kuzaga ameeleza kuwa gari hilo iliigonga kwa nyuma Gari yenye namba za usajili T.636 DQY aina ya Mitsubishi Rosa ikitokea Mbeya mjini kuelekea mbalizi ambalo lilikuwa likiendeshwa na dereva ,Elly Mwakalindile (41)mkazi wa Iyunga na kusababisha vifo vya watu Tisa ambapo kati yao wanaume watano na wanawake wanne.

Aidha  kamanda Kuzaga amesema kuwa katika ajali hiyo watu 23 walijeruhiwa kati  ambapo kati yao wanaume 13 na wanawake 10 ni majeruhi  na wanaendelea kutibiwa katika  Hospitali Teule ya Ifisi iliyopo Mji Mdogo wa Mbalizi na wengine wamehamishiwa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya.

 Miili ya marehemu imehifadhiwa Hospitali Teule ya Ifisi Mbalizi ambapo miili ya marehemu 07 imetambuliwa huku miili ya watu 02 ikiwa bado  haijatambuliwa.

Chanzo cha ajali hii ni Dereva wa lori kushindwa kulimudu gari lake kwenye mteremko mkali na kwenda kuigonga kwa nyuma Gari ya abiria na kuwa Dereva wa lori amekamatwa na atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa wito kwa madereva ambao wanapita katika Mkoa wa Mbeya kwenye milima na miteremko mikali kuhakikisha wanakagua magari yao kabla ya kuanza safari na wamiliki wa magari wasiruhusu magari yao kuendeshwa na madereva hao ili kuepusha ajali.

Tuesday 15 November 2022

November 15, 2022

TBS YAKUTANA NA WADAU WA VIWANGO KUHAMASISHA USHIRIKI KATIKA UANDAAJI VIWANGO

 Mkurugenzi wa bodi ya TBS, Dkt. Eliapenda Mariki akifungua warsha ya wadau kuhusu ushiriki katika uandaaji wa viwango iliyofanyika mapema jana Mkoani Morogoro. Baadhi ya washiriki wa warsha ya ushirikishwaji wa wadau katika uaandaji Viwango iliyofanyika mapema jana mkoani Morogoro 


**************************

Na Mwandishi Wetu, Morogoro

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) na wadau katika uandaaji wa viwango wameshauriwa kuongeza juhudi za kuoanisha viwango katika ngazi za kikanda na kushriki kikamilifu katika michakato wa kutayarisha viwango vya kimataifa ili kuziwezesha bidhaa kupenya kwenye masoko ya kimataifa.

Ushauri huo ulitolewa jana na Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya TBS, Dkt.Eliapenda Mariki, wakati akifungua warsha ya ushirikishwaji wa wadau katika uandaaji wa viwango nchini.

Warsha hiyo iliyofanyika mkoani Morogoro ilienda sambamba na Maadhimisho ya Siku ya Viwango Duniani Kwa mwaka 2022.

Dkt. Mariki alisema viwango vina mchango katika juhudi za dunia katika kufikia malengo endelevu (SDGs) kwani hutoa suluhisho halisi katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kimazingira.

Dkt. Mariki alisema mojawapo ya sababu zinazofanya bidhaa za nchi zinazoendela ikiwemo Tanzania kushindwa kupenya na kuingia kwenye masoko ya kimataifa ni kushindwa kwa bidhaa hizo kukidhi matakwa ya viwango.

"Wakati mwingine bidhaa hushindwa kuingia kwenye soko la kimataifa au la kikanda kutokana na tofauti za masuala ya matakwa ya kiwango cha bidhaa husika baina ya nchi na nchi na hatimaye" alisema Dkt. Mariki na kuongeza;

"Kwa sababu hii ni dhahiri kuwa iwapo kutakuwa na uoanishaji wa matakwa ya ubora baina ya nchi na nchi na hatimaye kuwa na viwango sawa kikanda na kimataifa, uwanja wa biashara utakuwa umesawazishwa."

Alifafanua kuwa viwango vina mchango mkubwa katika juhudi za dunia za kufikia malengo endelevu ya agenda 2030, kwani hutoa suluhisho halisi katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kimazingira.

Aliipongeza TBS kwa hatua ya kuwakutanisha wadau ili kuzungumza nao kuhusiana na ushiriki katika uandaaji wa viwango.

"Hii ni hatua muhimu katika msingi wa ushiriki wenye manufaa katika uandaaji wa viwango vya kitaifa, kikanda na kimataifa kwa manufaa ya nchi," alisema Dkt. Mariki.

Madhimisho hayo yalianza kufanyika nchini kuanzia Oktoba 22, mwaka huu kwa shughuli mbalimbali za kuelimisha umma juu ya umuhimu wa kushiriki mchakato wa uandaaji viwango kitaifa, kikanda na kimataifa.

Alisema kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ilibeba ujumbe usemayo;

" Viwango kwa Maendeleo Endelevu." Kwa mujibu wa Dkt. Mariki kauli mbiu hiyo inaendana na malengo ya maendeleo endelevu ambayo yanalenga kuweka usawa kijamii, kujenga uchumi endelevu na kupunguza kasi ya mabadliko ya tabia nchi.

Monday 14 November 2022

November 14, 2022

ORODHA YA WAGOMBEA CCM HII HAPA



Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) imekutana kikao cha kawaida Jumapili 13 Novemba, 2022 chini ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Samia Suluhu Hassan, Makao Makuu ya Chama, Dodoma.


Pamoja na mambo mengine, Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa imefanya uteuzi wa majina ya wanachama watakaogombea nafasi za uongozi ndani ya CCM na Jumuiya zake katika ngazi ya Mkoa na Taifa kwa mujibu wa katiba ya CCM ya mwaka 1977 Toleo la mwaka 2022 Ibara ya 82(1). Kwa upande wa wagombea wa nafasi ya Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya za CCM ngazi ya Taifa walioteuliwa ni kama ifuatavyo:-

 

 


NAFASI: MWENYEKITI UVCCM TAIFA

1.  Farid Mohamed HAJI

2.  Kassim Haji KASSU

3.  Mohamed Ali MOHAMED (KAWAIDA)

4.  Abdallah Ibrahim NATEPE

 

 

NAFASI: MAKAMU MWENYEKITI UVCCM TAIFA

1.  Khadija Khalid ISMAIL

2.  Dorice John MGETTA

3.  Victoria Charles MWANZIVA

4.  Rehema Sombi OMARY


NAFASI: MWENYEKITI UWT TAIFA

1.  Gaudentia Mugosi KABAKA

2.  Kate Sylvia KAMBA

3.  Dkt. Wemael Allen CHAMSHAMA

4.  Mariam Mohamed LULIDA

5.  Mary Pius CHATANDA

 

NAFASI: MAKAMU MWENYEKITI UWT TAIFA

1.  Latifa Nasser AHMED

2.  Thuwaybah Edington KISSASI

3.  Hafsa Said KHAMIS

4.  Zainab Khamis SHOMARI

 

NAFASI: MWENYEKITI WAZAZI TAIFA

1.  Dkt. CPA. Edmund Bernard MNDOLWA

2.  Fadhili Rajabu MAGANYA

3.  Bakari Nampenya KALEMBO

4.  Said Mohamed MOHAMED (DIMWA)

5.  Mwanamanga Juma MWADUGA

6.  Ally Maulid OTHMAN

7.  Ali Khamis MASUDI

8.  Hassan Haji ZAHARA

 

 

 

NAFASI: MAKAMU MWENYEKITI WAZAZI TAIFA

1.  Haidar Haji ABDALLA

2.  Dkt. Wemael Allen CHAMSHANA

3.  Fatma Abeid HAJI

4.  Rachel Ntiganyigwa KABUNDA

5.  Neema George MTURO

6.  Zahoro Salehe MOHAMED

7.  Dogo Idd MABROUK

 

Uchaguzi wa viongozi wa Jumuiya hizo kwa ngazi ya Taifa utafanyika tarehe 24-29 Novemba, 2022. Wagombea wote wanakumbushwa kuheshimu Kanuni za uchaguzi za CCM na misingi ya chama kwa kufanya siasa safi na kuzingatia maadili ya Chama wakati wote.


Aidha Orodha ya majina ya wagombea uongozi Chama na Jumuiya zake ngazi ya Mkoa yatatumwa katika mikoa husika.

 







Wednesday 9 November 2022

Tuesday 8 November 2022

November 08, 2022

CHAMA NA AZIZI KI WAPIGWA NYUNDO NA TFF.

 

Wachezaji Cletous Chama wa Simba sc na Stephane Aziz Ki wa Yanga sc wamefungiwa michezo mitatu na adhabu ya faini ya shilingi milioni tano kwa kosa la kutosalimiana na wachezaji wenzao katika mchezo wa ligi kuu uliozikutanisha klabu zao Oktoba 23 mwaka huu katika uwanja wa Benjamin Mkapa ambapo mchezo huo ulimalizika kwa sare ya 1-1.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na bodi ya ligi kuu nchini imesema kuwa wachezaji hao wamefungiwa kutokana na kuzingatia kanuni ya 41:5(5.4) ya ligi kuu kuhusu udhibiti wa wachezaji.

Kutokana na kufungiwa huku timu za Simba sc na Yanga sc zitaathirika sana kwa sababu wachezaji hao wamekua nguzo kubwa katika klabu hizo hasa katika kujenga mashambulizi na kupelekea kuwa na umuhimu mkubwa katika vikosi vya timu hizo huku Simba sc ikionekana kuathirika zaidi kutokana na kutokua na mbadala mwenye ubora wa kumfikia Chama katika eno analocheza.

Chama ataanza kuitumikia adhabu hiyo kesho ambapo klabu yake ya Simba sc itamkosa itakapocheza mchezo mkali na wa kusisimua dhidi ya Singida Big Stars katika uwanja wa Liti mkoani Singida ambapo tayari klabu ya Simba sc imeshawasili ambapo pia Chama ataikosa michezo mingine dhidi ya Ihefu na Namungo.

Stpehane Aziz Ki yeye ataikosa michezo dhidi ya Kagera Sugar ugenini siku ya Jumatatu pamoja na michezo dhidi ya Singida na ule wa Novemba 22 dhidi ya Dodoma jiji ugenini


Saturday 5 November 2022

November 05, 2022

KOSTROMA; DEADLY FIRE IN RUSSIAN BAR STARTES BY FLARE GUN

A fire in a bar in the Russian city of Kostroma has killed at least 13 people.



Authorities say it may have begun when a drunk customer at the nightclub fired a flare gun on the dance floor, Russian media report.

The fire reportedly spread when parts of the lighting rig on the ceiling ignited, quickly filling the room with smoke. It took several hours for it to be extinguished.

A suspect, said to be a local resident, has been arrested.

It took emergency workers several hours to put out the fire, which began at around 02:00 local time (23:00 GMT) in Kostroma, 300 km (180 miles) northeast of Moscow.

Russia's investigative committee said a 23-year-old man had been arrested on suspicion of using a "pyrotechnic" object inside the building which led to the fire.

The director of the company which manages the club has also been arrested.

Tass news agency quoted a law-enforcement source as saying that the suspected perpetrator had admitted responsibility.

"He was spending time with a woman, ordering flowers for her while he held a flare gun. Then he went to the dance floor and fired it," the source said.

The exact number of people inside the club at the time is not known, but 250 people were able to evacuate.

Images of the single-storey building engulfed in flames were shown on Russian state television, which said some safety measures had not been properly observed.

According to BBC Russian, the company which manages the club is owned by a local politician.

In 2009, 159 people died in a nightclub in the Russian city of Perm.


source BBC