DEAL PLUS

Karibu DEALPLUS BLOG uweze kupata habari za Michezo, Siasa, Afya na Burudani kutoka ndani na nje ya nchi.

Breaking


Sunday 18 June 2017

TIBA YA UGONJWA WA KUSAHAU

Sababu za tatizo la sahau mara nyingi hasababishwa na sababu zifuatazo:

-sumu katika mwili
-madawa
-ulevi
-ajali na hata urithi.

kwahiyo utabibu wako yategemea zaidi na sababu ya hilo tatizo lako.
kwanza jiangalie katika maisha yako hujawahi kupata ajali ambayo imepelekea ubongo kupata
mshtuko,utumizi wako wa madawa ukoje,jee ndani ya familia yako ni asilimia ngapi ya watu
wenye tatizo hilo,aina gani ya vyakula ambavyo unakula na wakati mwengine tatizo hili
husababishwa na sindikizo kubwa la mawazo ambalo huathiri ubogo

Fig tunda la Tini
Pendelea Kula tini (fig) mbili au tatu kabla ya Chakula (cha mchana na cha usiku).
Tini inayo calcium kwa wingi, pia inayo iron, copper, Zinc, Vit. C Vit. A (Lakini Vit A inapotea 30 percent kwa tini iliyo kauka.) Tini pia inayo Vit B (complex) na vit D.
Tini ni dawa nzuri sana kwa Wagonjwa wa kusahau.
Dawa nzuri nyingine ya wagonywa wa kusahau ni kulala masaa 8 kila siku (Usingizi wa usiku si kama usingizi wa mchana), usizidishe kulala zaidi ya masaa 8, kuzidisha pia ni mbaya kwa afya. Dawa zingine hizi hapa Utwange Dawa moja inayoitwa Halilinji Utwange upate unga wake uchanganye na Asali Safi mbichi ya nyuki
kijiko kimoja kikubwa uwe unakunywa kila siku katika maisha yako. Au ıpate Mafuta ya siku nyingi ya
Zaituni u jipake nyuma ya kichwa upande wa kichogoni uwe unajipaka kila siku inasaidia sana hayo mafuta ya Zaituni ya siku nyingi
Na ingine awe unakula Sana Figili na Samli Safi ya Ng'ombe.
itakusaidia kuondosha ugonjwa wa sahau. Au ule Zabibu kavu kwa wingi kila siku hiyo pia itakusaidia kuondosha huo ugonjwa wa Sahau.