DEAL PLUS

Karibu DEALPLUS BLOG uweze kupata habari za Michezo, Siasa, Afya na Burudani kutoka ndani na nje ya nchi.

Breaking


Thursday 19 August 2021

KODI YA MAJENGO KUANZA KULIPWA KWA NJIA YA UNUNUZI WA UMEME

 


Kupitia Mamlaka ya mapato Tanzani serikali imesema imeanza utekelezaji wa kukusanya kodi ya majengo kwa kutumia mfumo mpya wa ukusanyaji kupitia njia ya ununuzi wa umeme ,utekelezaji huo utaanza rasmi Agosti 20,2021 na unafanyika chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Mapato (TRA) kwa kushirikiana na TANESCO ukihusisha mita za aina zote za umeme.

Kwa njia hii ya ukusanyaji wa kodi kila mnunuzi wa umeme atakatwa kiasi cha Tsh. 1000 kwa mwezi kwa nyumba ya kawaida na Tsh.5000  kwa mwezi kwa kila sakafu ya ghorofa ,kwa wale wanaotumia mita za ankara watalipia kodi hii kwa pamoja katika Ankara ya mwezi.

No comments: