DEAL PLUS

Karibu DEALPLUS BLOG uweze kupata habari za Michezo, Siasa, Afya na Burudani kutoka ndani na nje ya nchi.

Breaking


Showing posts with label udokozi. Show all posts
Showing posts with label udokozi. Show all posts

Tuesday, 2 May 2017

May 02, 2017

NJIA ZA KUONDOA MAKOVU MWILINI NA KULAINISHA NGOZI YAKO

NJIA ZA KUONDOA MAKOVU MWILI NA KULAINISHA NGOZI YAKO

Makovu sio kidonda naomba hili uelewe,  ila makovu ni alama ya majeraha ambayo yamebaki kwenye ngozi baada ya kupona majeraha.

Kuna baadhi ya watu husumbuliwa na shida ya kuwa na makovu sehemu mbalimbali ya mwili.
Hivyo kama wewe ni miongoni mwao maandishi haya yanakuhusu sana.

Zifuatazo ndizo mbinu za kuondoa makovu mwilini.

1. Tango
Unachotakiwa kufanya ni; Pondaponda tango na kisha kutumia mchanganyiko wake kwa kupaka juu ya kovu. Hii husaidia sana kulainisha makovu na ikiwa utatumia kwa muda mrefu huondoa makovu pia.

2. Alo vera.
Unachotakiwa kufanya ni; kata majani hayo na utumie utomvu wake kupaka katika makovu kisha mara baada ya muda Fulani utaona mabadiliko na itapunguza na kuondoa makovu.

3. Asali
Unachotakiwa kufanya; Paka asali juu ya kovu na kuiacha usiku kucha. Rudia mara kwa mara kupaka asali hadi pale kovu litakapotoweka.

Monday, 1 May 2017

May 01, 2017

KAZI MPYA ZA RAYVAN ZINAZOTARAJIWA KUTOKA

Rayvanny azitaja kolabo zake zilizokuwa tayari

Msanii Rayvanny ametaja kolabo zake na wasanii wa nje ambazo zipo tayari.

Muimbaji huyo, ambaye yupo nchini Sweden kwa ziara yake ya muziki, amemuambia mmoja wa watangazaji wa nchi hiyo kua, tayari ameshafanya kolabo na msanii mkubwa kutoka Nigeria, Afrika Kusini na Kenya.

“Nina kolabo na msanii mkubwa kutoka Nigeria, ingawa kwa sasa siwezi kutaja jina lake. Lakini pia kuna kolabo Afrika Kusini, na Kenya ukiacha Bahati, kuna mwingine Khaligraph Jones kutoka Nairobi,” amesema Ray.

Kwa msanii wa Afrika Kusini tayari muimbaji huyo kutoka WCB ameshafanya kolabo na Dj Maphorisa tangu mwezi Disemba mwaka jana.

Friday, 28 April 2017

April 28, 2017

NDOA YA NUH MZIWANDA KUFUNGWA UPYA

Ndoa ya Nuh Mziwanda Kufungwa Upya

Ni siku moja tu imepita tangu staa wa Bongo Fleva Nuh Mziwanda kupitia account ya Instagram kupost picha ya mtoto wake aliyebarikiwa katika ndoa yake, inadaiwa ndoa hiyo kuingia katika mvutano. 

Inasemekana kuwa ndugu wa Nuh Mziwanda hawakuridhia ndoa ya ndugu yao iliyofungwa miezi kadhaa iliyopita kwa kuwa Nuh alibadili dini kufuata dini ya mke wake ambapo kupitia U-heard  ya XXL ya Clouds FM April 28 2017 mtangazaji Soudy Brown ameinasa sauti ya mke wa Nuh Mziwanda akimzungumza mama mkwe wake: 

“Nilimwambia mama unachelewa, mwambie aniache. Na anajua kuwa mimi sijaolewa na mwanawe, ila anajua nimezaa tu na mwanawe. Kwenye sherehe ya harusi hakuwepo, alikuwa kwenye msiba. Yule mama ni mzee wa Kanisa, alikuwa anataka niende kanisani nibadili dini ndio niolewe.” – Mama ANYA