DEAL PLUS

Karibu DEALPLUS BLOG uweze kupata habari za Michezo, Siasa, Afya na Burudani kutoka ndani na nje ya nchi.

Breaking


Monday 1 May 2017

SAIDA KAROLI ALILIWA NA AFANDE SELE

Saida karoli aliliwa na afande sele

Mfalme wa mashahiri bongo, Afande Sele amefunguka kwamba watanzania kuupotezea muziki wa Saida Karoli na kusapoti muziki unaokopiwa kutoka mataifa mengine ni kupoteza uhalisia wa Kitanzania.

Afande Sele amefunguka hayo karibuni  na kusema Saida ni msanii ambaye ana uhalisia wa Tanzania na kipaji hivyo hakupaswa kupotea kwenye soko la muziki, Watanzania wanapaswa kuendelea kumshika mkono na kutomtelekeza.

"Muziki ni kipaji na Saida anacho. Saida Karoli ni hazina kwanza ni muimbaji ambaye anaitambulisha nchi yetu kwa nyimbo za asili tofauti na wasanii wengine wote waliopo kwenye 'game'. Sijaona mtu wa kumfananisha nae lakini kwa sababu wamekuja watu wengine ndiyo wanaonekana wakifanya vizuri kuliko yeye kumbe siyo"- alisema Afande.

Aidha Afande ameendelea kuongeza kwamba " Umri siyo tatizo katika uimbaji bali kipaji cha kweli huwa hakipotei haraka kama jinsi ambavyo Saida amekuwa kimya, hebu mpeni nafasi tena kwenye muziki huu ili akapeperushe bendera ya nchi".- Afande Sele.

Katika hatua nyingine Afande amewaasa wasanii kudumisha upendo kitu ambacho ni silaha ambayo wao kama wakongwe ndiyo iliweza kuwasaidia katika kipindi chote walipokuwa wanafanya sanaa.

No comments: